9 Umufundishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima; umufundishe mutu wa haki naye atazidi kuwa na elimu.
Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
Onyo la mwenye hekima kwa mutu musikilivu ni bora kuliko pete au ushanga wa zahabu safi.
Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
Lakini muzidi kukomaa katika neema na katika kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Asifiwe, sasa na hata milele! Amina.
Ninawaandikia maneno yale, ninyi wenye kuamini kwa jina la Mwana wa Mungu, mupate kujua kwamba muko na uzima wa milele.