Yosefu alipomwona Benjamina pamoja nao, akamwambia musimamizi wa nyumba yake: “Uwapeleke watu hawa kwenye nyumba, uchinje nyama mumoja na kumutengeneza vizuri, maana watu hawa watakula nami chakula cha muchana.”
Ningekuongoza na kukufikisha ndani ya nyumba ya mama muzazi, pahali ambapo ungenifundisha upendo. Ningekupa divai nzuri iliyokolezwa, ningekupa divai yangu ya makomamanga yangu.
Juu ya mulima Sayuni, Yawe wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya nyama zenye kunona na divai nzuri, nyama tamu zenye mafuta, pamoja na divai safi.