9 Kwa mutu mwenye ufahamu kila kitu ni wazi, kwa mwenye maarifa yote imesawanishwa.
Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.
Mwenye akili anatafuta maarifa, lakini wapumbafu wanajikulisha upumbafu.
Njia ya mwenye hekima inaelekea juu kwenye uzima, kusudi aepuke kuingia chini katika kuzimu.
Hekima ni mbele ya uso wa mwenye akili, lakini macho ya mupumbafu yanaangalia kwa miisho ya dunia.
Mutu mwenye akili anajipatia maarifa; sikio la mwenye hekima linatafuta maarifa.
Heri mutu anayetambua hekima, mutu yule anayepata ufahamu.
Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,
Inafaa kusema hivyo, enyi wazao wa Yakobo? Yawe ameacha uvumilivu wake? Yeye anafanya mambo kama haya? Maneno yangu yanawafalia wenye mwenendo sawa.
Imeandikwa hivi katika maandiko ya manabii: ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mutu anayemusikia Baba na kufuata mafundisho yake, anakuja kwangu.
Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.
Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.