32 “Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.
Maana nimefuata njia za Yawe, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa ajili ya uovu.
Shimo la kuangamia na Kifo wanasema: “Tumesikia uvumi wake kwa masikio yetu.”
Wimbo wa safari za kidini. Heri wote wanaomwabudu Yawe, wanaoishi kufuatana na amri zake.
Yawe alinitendea kwa kadiri ya haki yangu; alinilipa kwa vile mikono yangu haina kosa.
Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria.
Heri mutu anayetambua hekima, mutu yule anayepata ufahamu.
Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.
Sasa enyi wana wangu, musikilize, wala musisahau maneno ya kinywa changu.
Sasa wana wangu, munisikilize; mutege sikio kwa maneno ya kinywa changu.
Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”