19 Matunda yangu ni mazuri kuliko zahabu safi, na faida yangu inashinda ya feza bora.
Hekima haiwezi kupatikana kwa zahabu, wala kwa kupima kiasi kingi cha feza.
Topazi ya Etiopia haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kupewa bei ya zahabu safi.
Maneno ya mwenye haki ni kama feza bora. Akili ya mutu mwovu haifai kwa kitu chochote.
Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.
Hekima ni bora kuliko feza, ina faida kuliko zahabu.
Chagua mafundisho yangu pahali pa feza; na maarifa pahali pa zahabu safi.
Ninatembea katika njia ya haki; ninafuata sheria ya Mungu.
Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.