Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Nina uwezo wa kushauri na kuamua vizuri. Nina ufahamu na nina nguvu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 8:14
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hekima na uwezo ni vya Mungu. Yeye ana maarifa na ujuzi.


mumetupilia mashauri yangu yote, mumezarau maonyo yangu.


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.


Kuwa na hekima na maarifa ni bora kuliko kuwa na nguvu.


Mwana wangu, shika hekima safi na akili; usiviache vitoweke mbele ya macho yako,


Hekima inamufanya mwenye hekima kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi katika muji.


Ujuzi huu nao unatoka kwa Yawe wa majeshi. Mipango yake ni ya ajabu, hekima yake ni kamilifu kabisa.


Yawe alitaka shauri toka kwa nani, halafu akapata kuwa mwenye akili? Nani aliyemufundisha kuhukumu kwa haki? Nani aliyemufundisha maarifa, na kumwonyesha namna ya kuwa na akili?


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Wewe unapanga kwa hekima na unafanya maajabu; njia za watu wote ziko wazi mbele yako, unamulipa kila mumoja kadiri ya njia zake na matendo yake.


Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.


Wanajidai kwamba wao ni wenye hekima, lakini wako wapumbafu.


Lakini kwa wale walioitwa na Mungu, ikiwa Wayuda au wasiokuwa Wayuda, Kristo ni kitambulisho cha uwezo na hekima ya Mungu.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ