11 “Hekima ina maana sana kuliko mawe ya bei kali; kitu chochote unachotamani hakiwezi kulingana nayo.
Maagizo yako ni matamu sana kwangu; ni matamu kuliko asali!
Kweli, ninapenda amri zako, kuliko hata zahabu safi kabisa.
Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.
Kumutii Yawe ni jambo jema; kunadumu milele. Maagizo ya Yawe ni sawa, yote ni ya haki kabisa.
Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.
Kuna zahabu na wingi wa mawe ya bei kali; lakini kitu cha bei kali zaidi ni maneno ya maarifa!
Muke mwema atapatikana wapi? Bei yake ni kali kuliko ushanga!
Hekima ni ya bei kubwa kama urizi; ni ya mafaa kwa wale wote wanaokuwa wazima.
Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.
Wala haziko ngambo ya bahari, hata museme: ‘Nani atakayevuka bahari atuletee kusudi tuzisikie na kuzitii.’