Nyoka alikuwa mwerevu kuliko nyama wote wa pori walioumbwa na Yawe Mungu. Basi, nyoka akamwambia yule mwanamuke: “Ni kweli Mungu alisema musikule matunda ya muti wowote katika bustani?”
Yehu alipofika Yezereheli, Yezebeli alikuwa amekwisha kupata habari ya mambo yaliyotokea. Alijipakaa rangi kwenye macho na kuchanua nywele zake, kisha akaenda kwenye dirisha na kuangalia chini.
Kamata kinubi chako uzungukezunguke ndani ya muji, ewe kahaba uliyesahauliwa! Imba nyimbo tamutamu. Imba nyimbo nyinginyingi, kusudi upate kukumbukwa tena.
Nawe Yerusalema uliyeachwa tupu, kwa nini sasa unavaa nguo nzuri nyekundu? Kwa nini kujipamba kwa zahabu, na kujipakaa wanja kwenye macho? Unajipamba bure! Wapenzi wako wanakuzarau sana; wanatafuta kukuua tu.
Ninataka vilevile wanawake wavae kwa namna inayostahili. Inafaa wajipambe kwa adabu na kwa ukadirifu, si kwa namna mbalimbali za urembo za kusuka nywele, wala kwa zahabu, wala kwa ushanga au nguo za bei kali.