Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Ewe muvivu! Kwenda kuchunguza siafu, fikiri juu ya namna yake ya kuishi upate hekima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 6:6
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutego unaotegwa na ndege akiona, mutego ule unategwa bure.


Kama vile siki inavyokuwa kwa meno au moshi ndani ya macho, ndivyo muvivu anavyokuwa kwa bwana wake.


Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.


Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.


Njia ya muvivu inajaa miiba, lakini njia ya mutu wa usawa ni wazi kama barabara kubwa.


Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.


Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.


Muvivu anatia mukono wake katika sahani lakini hauinui mpaka kwenye midomo.


Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.


Muvivu anakufa kwa kutokutimizwa kwa tamaa zake, maana mikono yake haitaki kufanya kazi.


Muvivu anasema: “Kuna simba inje. Nitauawa katika njia.”


Sikia, mwana wangu, ukuwe na hekima; fikiri sana jinsi unavyoishi.


Kuna viumbe vine vidogo sana katika dunia, lakini vina akili sana:


siafu ni wadudu wasiokuwa na nguvu, lakini wanajiwekea chakula wakati wa kipwa;


Ewe muvivu, utalala pale mpaka wakati gani? Utaamuka wakati gani katika usingizi wako?


Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!


Hata korongo anajua wakati wa kuhama; njiwa, mbaruwayi na koikoi, wanajua nyakati zao za kurudi. Lakini hawa watu wangu hawajui maagizo ya Yawe.


Naye bwana wake akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya na muvivu! Ulijua kama ninavuna nafasi nisipopanda, na kukusanya nafasi nisiposambaza.


Muangalie ndege wanaoruka katika anga: wao hawapandi mbegu wala hawavuni, wala hawaweki mavuno ndani ya gala, lakini Baba yenu anayekuwa mbinguni anawakulisha! Basi ninyi si wa lazima zaidi kuliko ndege wale?


Musikuwe wavivu katika kazi lakini mukuwe na bidii, mukimutumikia Bwana kwa juhudi.


Basi musigeuke kuwa wavivu, lakini mufuate mufano wa wale wanaoamini na kuvumilia. Kwa njia hiyo wanapokea yale Mungu aliyoahidi kuwapa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ