Mezali 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzako, lakini mwana wangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi: umwendee mutu yule mara moja, umusihi akupe uhuru wako.
Kisha Nabii Semaya akamwendea mufalme Rehoboamu na wakubwa wa Yuda, waliokusanyika Yerusalema ambapo walikimbilia kwa kumwepuka Sisaki, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Ninyi mumeniacha mimi, kwa hiyo basi, nami nimewaacha ninyi na kuwatia katika mikono ya Sisaki.’ ”
Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.