Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 6:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 6:23
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yosefu akakataa na kumwambia yule muke wa bwana wake: “Sikiliza! Bwana wangu amenipa mamlaka juu ya kila kitu hapa ndani ya nyumba na hajishugulishi na kitu chochote tena.


Neno lako ni taa ya kuniongoza, na mwangaza katika njia yangu.


Maelezo ya mafundisho yako yanaleta mwangaza; yanawapa akili wajinga.


Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.


Sheria ya Yawe ni kamilifu; inamupa mutu uzima mupya. Maagizo ya Yawe ni ya kuaminiwa; yanawapa wajinga hekima.


Anayekubali kufundishwa anaelekea kwenye uzima, lakini anayekataa kuonywa amepotoka.


Njia ya mwenye hekima inaelekea juu kwenye uzima, kusudi aepuke kuingia chini katika kuzimu.


Mutu ambaye anasikiliza maonyo mema ana nafasi yake kati ya wenye hekima.


Azabu na maonyo vinaleta hekima, lakini mutoto aliyeachiliwa anapatisha mama yake haya.


Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.


Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.


Baba yangu alinifundisha hiki: “Shika kwa moyo maneno yangu, shika amri zangu nawe utaishi.


Kwa hiyo utasema: “Kwa nini nilichukia mafundisho? Kwa nini nilizarau ndani ya moyo wangu?


Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.


Afazali kusikia maonyo ya wenye hekima kuliko kusikiliza nyimbo za wapumbafu.


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Nawe Yeremia utawaambia watu hawa kwamba: Yawe anasema hivi: Musikilize! Mimi ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo.


Niliwapa masharti yangu na kuwafundisha maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi.


Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi.


Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.


Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ