6 Yeye haijali njia ya uzima, njia zake ni za kutangatanga, wala hajui.
Nimefikiri juu ya mwenendo wangu, na nimerudi nifuate maagizo yako.
Unanionyesha njia ya kufikia uzima. Kuwa mbele yako ni kujazwa furaha, kuwa kwa kuume kwako kunapendeza milele.
Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.
Yeyote anayemwendea harudi hata kidogo, wala harudilii tena njia ya uzima.
Mwenendo wa mwanamuke mwasherati ni hivi: yeye anakula, anajipanguza mudomo, na kusema: “Sijafanya kosa lolote!”
Chunguza sana njia utakayopitia, na hatua zako zote zitakuwa kamili.
Maana mwenendo wa kila mutu ni wazi mbele ya Yawe; yeye anachunguza njia zake zote.
Mwanamuke mupumbafu ana kelele, hajui kitu wala hana haya.
Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!