3 Midomo ya mwanamuke mupotovu ni mitamu kama asali, maneno yake ni laini kuliko mafuta;
Mwenzangu amemushambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.
Utaepukana na mwanamuke mwasherati, mwanamuke kahaba wa maneno matamu,
Kinywa cha mwasherati ni shimo refu; anayechukiwa na Yawe atatumbukia ndani yake.
Mwana wangu, kwa nini kutekwa na mwanamuke mwasherati? Kwa nini kukumbatia mwanamuke mugeni katika kifua?
Yatakulinda mbali na mwanamuke mubaya, yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamuke mugeni.
Alimushawishi kwa maneno mengi ya kubembeleza; kijana akashawishiwa kwa maneno yake matamu.
Vitakulinda mbali na mwanamuke mubaya, vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamuke mugeni.
Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.
Midomo yako inadondosha asali, ee muchumba wangu, ulimi wako una asali na maziwa. Harufu nzuri ya nguo zako ni kama miti ya Lebanoni.