16 Kwa nini chemichemi zako zitawanywe mbali, na vijito vya maji katika barabara?
Basi, wakamubariki Rebeka wakisema: “Ewe dada yetu! Ukuwe mama wa maelfu kwa maelfu; wazao wako warizi miji ya waadui zao.”
Watoto ni urizi kutoka kwa Yawe; uzao ni zawadi yake kwetu sisi.
Muke wako atakuwa kama muzabibu wenye matunda mengi; watoto wako kama vichipukizi vya muzeituni kuzunguka meza yako.
Mbele waimbaji, nyuma wanamuziki, katikati wabinti wanavumisha ngoma.
Kunywa maji ya birika lako mwenyewe, maji yanayobubujika katika kisima chako mwenyewe.
Hiyo ni yako wewe mwenyewe, wala usiwashirikishe watu wengine.
Chemichemi yako ibarikiwe, umufurahie muke uliyemwoa ukiwa kijana.
“Maji yaliyoibwa ni matamu sana; mukate unaokuliwa kwa siri ni muzuri sana.”
Dada yangu, muchumba wangu, ni bustani yangu ya pekee, chemichemi inayochungwa.
Wewe ni chemichemi ya bustani, kisima cha maji yasiyokauka, vijito vinavyotiririka kutoka milima ya Lebanoni.
Alipowaongoza katika jangwa hawakuona kiu, aliwatiririshia maji kutoka katika jiwe, alipasua jiwe maji yakabubujika.
Kwa hiyo, watu wa Israeli wakakaa salama, wazao wa Yakobo peke yao, katika inchi iliyojaa ngano na divai, inchi ambayo anga lake linadondosha umande.
Yeye alikuwa na wana makumi tatu na wabinti makumi tatu. Nao wabinti zake aliwaoesha inje ya ukoo wake, na wana aliwaoea wabinti makumi tatu kutoka inje ya ukoo wake. Ibusani alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka saba.