Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 4:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana mule munatokea chemichemi za uzima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 4:23
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yehu hakutii sheria za Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Mwanamuke mwema anaheshimiwa; wanaume wenye nguvu wanatajirika.


Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.


Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.


Njia ya waovu imejaa miiba na mitego; anayetaka kulinda maisha yake ataiepuka.


Sikia, mwana wangu, ukuwe na hekima; fikiri sana jinsi unavyoishi.


Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mupumbafu; lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.


Mwana wangu, shika hekima safi na akili; usiviache vitoweke mbele ya macho yako,


Jambo la musingi ni kujipatia hekima; toa vyote unavyokuwa navyo ujipatie akili.


Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Lakini vyote vinavyotoka ndani ya kinywa ni vyenye kutoka kwanza ndani ya moyo wake, navyo vinamuchafua mutu.


Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano.


Mukeshe na kuomba, kusudi musianguke katika majaribu; kwa maana roho ni hodari, lakini mwili ni zaifu.”


Mutu muzuri anasema maneno mazuri kutokana na uzuri wa moyo wake. Na mutu mubaya anasema maneno mabaya kutokana na ubaya wa moyo wake. Kwa maana kinywa cha mutu kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo wake.


“Lakini mukuwe waangalifu na kufanya angalisho sana kusudi musisahau mambo yale muliyoona kwa macho yenu wenyewe, kusudi isitokee hata mara moja katika maisha yenu mambo hayo kusahaulika ndani ya mioyo yenu. Muwaelezee watoto wenu na wajukuu wenu


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ