22 Maana hayo ni uzima kwa mutu anayeyapata, ni dawa kwa mwili wake wote.
Maneno ya ovyo yanaumiza kama upanga, lakini kusema kwa mwenye hekima kunaponyesha kidonda.
Maneno mazuri ni kama asali. Ni matamu kwa nafsi na yenye kuupatia mwili afya.
navyo vitakuwa uzima katika nafsi yako, na pambo zuri katika shingo lako.
Hiyo itakuwa dawa kwa mwili wako, na kitu cha kutuliza mifupa yako.
Mwana wangu, sikia na kupokea maneno yangu, kusudi upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.
Baba yangu alinifundisha hiki: “Shika kwa moyo maneno yangu, shika amri zangu nawe utaishi.
Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.
Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.