20 Mwana wangu, sikia kwa uangalifu maneno yangu, utegee sikio masemi yangu.
Mukuje, enyi vijana munisikilize, nami nitawafundisha kumwabudu Yawe.
Mashairi ya Asafu. Musikie mafundisho yangu, enyi watu wangu, mutegee sikio maneno ya kinywa changu.
Utufundishe ufupi wa maisha yetu kusudi tuweze kuwa na hekima.
ukitega sikio lako kwa kusikiliza hekima, na kuelekeza moyo wako upate ufahamu,
Wewe utafurahi kama utayaweka ndani ya moyo, na kuyarudiliarudilia kila wakati.
Mwana wangu, sikia hekima yangu, tega sikio usikie elimu yangu.
Mwana wangu, ushike maneno yangu, uchunge amri zangu.
Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.
Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”