Kila mutu anadanganya jirani yake, hakuna hata mumoja anayesema ukweli. Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo; anatenda uovu kwa kadiri ya kushindwa kabisa kunigeukia.
Yawe anasema hivi juu ya manabii wanaowapotosha watu wake, manabii ambao wanatabiri amani wakipewa kitu, lakini wanawatishia watu kwa vita wasipopewa kitu:
Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [