Waisraeli walipoona kitu kile wakashangaa, wakaulizana: “Nini hii?” Hawakujua kilikuwa kitu gani. Basi, Musa akawaambia: “Huu ni mukate ambao Yawe amewapa mukule.
Lakini wote walipopima kiasi walichookota katika kipimo cha litre ine, walitambua kwamba aliyeokota kingi hakukuwa na cha zaidi na aliyeokota kidogo, hakupungukiwa. Kila mumoja alikuwa ameokota kiasi alichoweza kula.
Mufahamu kwamba mimi Yawe nimewapa siku ya Sabato, ndiyo maana nimewapa chakula cha siku mbili kwa siku ya sita. Basi, kila mutu apumzike ndani ya nyumba yake. Mutu yeyote asitoke katika siku ya saba.”
Hakuna anayemushitaki mwenzake kwa haki, wala anayejitetea kwa ukweli. Munategemea mambo ya bure; munasema uongo. Munafanya mipango ya kuleta hasara na kuzaa uovu.
Basi, mufalme Zedekia akatoa amri Yeremia awekwe katika chumba cha walinzi na kupewa mukate kila siku kutoka kwa wapikaji wa mukate mpaka mikate ilipotoweka kabisa huko katika muji. Basi, Yeremia alibaki katika chumba cha walinzi.
“Wandugu, kwa sababu gani munafanya mambo kama haya? Sisi vilevile ni watu, tuko sawasawa nanyi, na tunawahubiri ninyi Habari Njema kwamba muache kuabudu vitu hivi vya bure na mumugeukie Mungu mwenye uzima; yeye aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao.