Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 30:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 30:4
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mutu akamwambia: “Hautaitwa Yakobo tena, lakini Israeli, kwa sababu umeshindana na Mungu na wanadamu, ukashinda.”


Unaweza kuvumbua siri za Mungu na kujua ukomo wa Mungu Mwenye Uwezo?


Ukubwa wake unapita mbingu; wewe unaweza nini? Kimo chake kinapita kuzimu; wewe unaweza kujua nini?


Anayafunga maji katika mawingu yakuwe mazito, nayo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.


Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia, anapiga umeme na kunyesha mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Wamasikini watakula na kushiba; wanaomutafuta Yawe watamusifu. Mungu awajalie waishi milele!


Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari; aliisimika imara juu ya maji mengi.


Bwana anakuja kwenye pahali pake patakatifu kutoka Sinai, akikuwa na kundi kubwa, na maelfu na maelfu ya magari ya kukokotwa.


Lakini wewe uliuvumisha upepo wako, nayo bahari ikawafunika. Walizama ndani ya maji kama risasi.


Nilimutokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo nikijulikana kama Mungu Mwenye Nguvu, ingawa sikuwajulisha jina langu, Yawe.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Alikamatwa kwa kinguvu, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa; na hakuna mutu aliyejali mambo yanayomupata. Alifukuzwa kutoka inchi ya wanaokuwa wazima, kwa sababu ya makosa ya watu wangu.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


Lakini hivi ndivyo inavyosemwa juu ya kuhesabiwa haki kwa njia ya imani: “Usijiulize: ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’ ” (maana yake ni kumushusha Kristo toka kule.)


“Kama musipokuwa waangalifu kwa kushika maneno yote ya sheria hii iliyoandikwa katika kitabu hiki na musipoheshimu na kutukuza jina tukufu la kuogopesha la Yawe, Mungu wenu


Haziko mbinguni hata museme: ‘Nani atakayepanda juu mbinguni kutuletea kusudi tupate kuzisikia na kuzitii?’


Macho yake yalimetameta kama ndimi za moto, na juu ya kichwa chake kulikuwa taji nyingi. Alikuwa na jina lililoandikwa juu yake, wala hakuna mutu aliyejua, isipokuwa yeye mwenyewe tu.


Malaika wa Yawe akamujibu: “Kwa nini unataka kujua jina langu? Ni la ajabu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ