Azaria, Kuhani Mukubwa aliyekuwa wa uzao wa Sadoki akamujibu: “Tangu wakati watu walipoanza kuleta matoleo yao katika hekalu, tumekuwa na vyakula vya kutosha na hata tuna akiba kubwa. Yawe amewabariki watu wake, ndiyo maana tumepata vitu hivi vyote.”
Kila kazi aliyoifanya katika utumishi wa nyumba ya Mungu au katika kutii sheria na amri za Mungu kwa kufuata uongozi kutoka kwake, alizifanya kwa moyo wake wote, naye akafanikiwa.
Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.
Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu.
Hamujaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa sadaka zenu. Nami sikuwalemea ninyi kwa kutaka sadaka, wala sikuwachokesha kwa kuwadai ubani.
Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.
Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.