Kisha, Daudi akasimama, akaoga, akajipakaa mafuta na kubadilisha nguo zake. Halafu akaenda katika nyumba ya Yawe na kuabudu. Kisha akarudi kwake, akaamuru wamuletee chakula, naye akakula.
Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.
Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.