4 Hivyo utakubaliwa na kusifiwa, mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.
Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kumutendea mema, hata kumufanya apate kukubaliwa mbele ya mukubwa wa kifungo.
Kumwogopa Yawe ni musingi wa hekima; wote wanaotii amri zake wanajaliwa akili. Sifa zake zinadumu milele.
Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.
Kuwa na akili kunaleta ukubali, lakini njia ya waovu ni ya taabu.
Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.
Basi, Mungu akamujalia Danieli kupendelewa na kuhurumiwa na Aspenazi, yule mukubwa.
Na Yesu alizidi kuwa na hekima, na kuongezeka kimo na kuendelea kumupendeza Mungu na watu.
Nao walisifu Mungu na kufurahiwa na watu wote. Na kila siku Bwana aliongeza katika kundi la waamini watu waliokuwa wakiokolewa.
Na yeyote anayemutumikia Kristo kwa njia hiyo anamupendeza Mungu, naye anapata kuwa mwenye kustahili mbele ya watu.
Kwa maana tunataka kufanya mema, si mbele ya Bwana tu, lakini mbele ya watu vilevile.
Yawe alimusikilia Hana huruma naye akajaliwa kupata watoto wa kiume watatu na wabinti wawili. Mutoto Samweli akaendelea kukomaa mbele ya Yawe.
Mutoto Samweli aliendelea kukomaa, akazidi kupendwa na Yawe na watu.