Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wema na uaminifu zisitengane nawe. Uvifunge katika shingo lako; uviandike ndani ya moyo wako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 3:3
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe ulikuja huku juzijuzi tu. Nikufanye mutu wa kutangatanga pamoja nasi, nikijua kwamba sijui hata kule ninakokwenda? Rudi pamoja na wandugu zako. Naye Yawe akuonyeshe wema na uaminifu.”


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Njia zote za Yawe ni njema na za uaminifu kwa wale wanaoshika agano lake na maagizo yake.


Hakika yeye ni tayari kuwaokoa wanaomuheshimu, na utukufu wake utadumu katika inchi yetu.


Na mambo haya yatakuwa ukumbusho, kama vile kitambulisho katika mikono yenu au katika paji la nyuso zenu; kusudi kiwakumbushe siku zote sheria ya Yawe. Maana, Yawe amewatoa katika inchi ya Misri kwa mukono wenye nguvu.


Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena: Yawe, Yawe, ni Mungu mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa wema na uaminifu.


hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako, kama mukufu katika shingo yako.


Anayepanga kutenda maovu kweli anakosa! Wanaopanga kutenda mazuri watapata mema na uaminifu.


Kwa wema na uaminifu mutu anaondoa uovu. Kwa kumwogopa Yawe anaepuka ubaya.


Wema na uaminifu unamukinga mufalme; utawala wake unaimarishwa kwa haki.


uyaweke siku zote ndani ya moyo, uyafunge katika shingo lako.


Uyafunge kwenye vidole vyako; uyaandike ndani ya moyo wako.


Zambi ya watu wa Yuda, haiwezi kufutikana, imeandikwa kwa kalamu ya chuma; kwa chongo ya almasi. Imechorwa ndani ya mioyo yao na kwenye pembe za mazabahu yao.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Mafundisho yao yalikuwa ya kweli nao hawakufundisha uongo hata kidogo. Mimi na wao tulikaa kwa amani. Si kwamba walitenda haki tu, lakini waliwafundisha wengine kutotenda maovu.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula, lakini mumeacha mambo makubwa yanayoamuriwa na Sheria, kama vile haki, huruma, na uaminifu. Mambo hayo ndiyo muliyopaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Inaonekana wazi kwamba ninyi ni barua iliyoandikwa na Kristo na kutumwa kwa njia ya utumishi wetu. Barua hii inaandikwa si kwa wino, lakini kwa Roho wa Mungu Mwenye Uzima. Barua hiyo haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, lakini katika mioyo ya watu.


kwa maana matunda ya mwangaza ni wema wa kila namna, haki na ukweli.


Muyafunge katika mikono yenu na kuyavaa katika paji za nyuso zenu kama vile ukumbusho.


“Hili ndilo agano nitakalofanya nao nyuma ya siku zile. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri, nikiziandika ndani ya mioyo yao.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ