26 maana Yawe ndiye atakayekutegemeza, atakuepusha usipate kunaswa katika mutego.
Kumwogopa Mungu si ndilo tegemeo lako? Na ukamilifu wa mwenendo wako si ndilo tumaini lako?
Hatakuacha uanguke; mulinzi wako hasinzii.
Hakika Mungu atakuokoa katika mutego, atakukinga na magonjwa mabaya.
Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.
Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.