Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.
Miti inayokuwa katika mashamba itazaa matunda, udongo utatoa mazao kwa wingi, nao wataishi kwa salama katika inchi yao. Nitakapovunja nira zao za utumwa na kuwaokoa toka katika mikono ya hao waliowafanya kuwa watumwa halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Usiku, mbele ya kutimia kwa siku Herode aliyotaka kumusambisha mbele ya watu, Petro alikuwa amelala ndani ya chumba katikati ya waaskari wawili. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili, nao walinzi walikuwa wakichunga mulango wa kifungo.