Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 3:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 3:18
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya.


Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”


Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.


Tumaini la kungojangoja linaumiza moyo, lakini tazamio linalotimia ni musingi wa uzima.


Ulimi mupole ni musingi wa uzima, lakini uovu wake unavunja moyo.


Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.


“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.


Heri mutu anayenisikiliza, anayeikaa kila siku kwenye mulango wangu, anayekesha karibu na milango yangu.


Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!


Muto ule ulitelemuka katikati ya barabara ya muji mutakatifu. Kandokando ya ule muto, kulikuwa kumeota muti wa uzima, nao unatoa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, maana yake mara moja kila mwezi. Majani ya muti ule yanatumiwa kama dawa ya kuponyesha mataifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ