Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 27:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mutu aliyepotea mbali na kwake ni kama ndege aliyepotea mbali na chicha yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 27:8
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.


Kisha Kaina akaondoka mbele ya Yawe, akaenda kuishi katika inchi ya Nodi, upande wa mashariki wa Edeni.


Lakini mufalme wa Misri akamwuliza: “Nimekunyima nini hata uamue sasa kurudi katika inchi yako?” Naye Hadadi akasema: “Uniache tu niende.”


Kule, akafika kwenye pango, akakaa mule. Mara moja Yawe akamutolea ujumbe: “Elia! Unafanya nini hapa?”


Anayetangatanga mbali na njia ya ufahamu, atajikuta ametua kati ya wafu.


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Aliyeshiba anakataa hata asali, lakini kwa mwenye njaa kila chakula kichungu ni kitamu.


Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka, wakiwa wamefukuzwa kutoka chicha zao, ndivyo wabinti wa Moabu wanavyokuwa kwenye vivuko vya Arnoni.


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Inafaa kila mutu abaki sawa alivyokuwa wakati alipoitwa na Mungu.


Wanafanana na zoruba kubwa ya bahari na matendo yao ya haya yanaonekana kama pofu ya zoruba. Wanafanana vilevile na nyota zinazotangatanga; Mungu amekwisha kuwawekea nafasi katika giza kubwa kwa milele.


Kisha nabii Gadi akamwambia Daudi: “Usikae hapa katika makimbilio. Ondoka mara moja uende katika inchi ya Yuda.” Basi, Daudi akaondoka, akaenda katika pori la Hereti.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ