6 Makaripio ya rafiki yanaonyesha uaminifu, lakini busu la adui ni udanganyifu.
Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.
Anayemuchukia mwingine kwa siri ni munafiki. Anayemusingizia mutu ni mupumbafu.
Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu; fimbo inasafisha nafsi mpaka ndani kabisa.
Aliyeshiba anakataa hata asali, lakini kwa mwenye njaa kila chakula kichungu ni kitamu.
Anayemwonya mwenzake kwa mwisho atasifiwa naye, kuliko yule anayemubembeleza kwa maneno matamu.
Wababa zetu wa kimwili walituadibisha kwa siku chache kufuatana na vile walivyoona kuwa vema. Lakini Mungu anatuadibisha kwa mafaa yetu kusudi tupate kushirikiana naye katika utakatifu wake.
Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.