5 Umujibu mupumbafu kama kufuatana na upumbafu wake, kusudi asijione kuwa mwenye hekima zaidi.
Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.
Usimujibu mupumbafu kipumbafu, kusudi usifanane naye.
Kutuma ujumbe kwa mukono wa mupumbafu ni kama kujikata miguu au kujitafutia mateso.
Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima, lakini masikini mwenye akili atamufichua.
Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima; umwogope Yawe na kujiepusha na uovu.
Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.
Nao walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka na kuwaambia: “Mutu asiyekuwa na zambi kati yenu, akuwe wa kwanza kumutupia jiwe.”
Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.
Mukuwe na masikilizano kati yenu. Musikuwe na nia ya kujitukuza, lakini mukubali kuishi katika unyenyekevu. Musijiwazie kuwa wenye akili sana.
Ushuhuda huo ni wa kweli. Basi kwa hiyo uwaonye vikali, kusudi wapate kuwa na imani kamili.