Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munafanana na makaburi yaliyopakaliwa chokaa, yanayoonekana kuwa mazuri kwa inje, lakini ndani yanajaa mifupa ya wafu na uchafu wa kila namna.