20 Bila kuni, moto unazimika; bila mwenye kuchochea, ugomvi unamalizika.
Mutu mupotovu anatawanya ugomvi, na muchonganishi anatenganisha warafiki.
Umufukuze mwenye kiburi na fujo itatoweka, na ugomvi na matusi vitakoma.
Maneno ya muchongeaji ni kama chakula kitamu; yanashuka mpaka ndani kabisa ya tumbo.
Usipitepite hata kidogo ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usitie maisha ya mwenzako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ni Yawe.
Hivi vilevile ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini unaweza kujivunia mambo makubwa sana. Muangalie, moto kidogo inaweza kuchoma pori kubwa sana!
Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.