19 ndivyo mutu ambaye anadanganya jirani, kisha anasema: “Nilikuwa ninafanya muzaha tu!”
Kwa mupumbafu, kutenda maovu ni kama muchezo, lakini watu wenye akili wanafurahia hekima.
Wapumbafu wanafurahia zambi, lakini watu wa usawa wanapata rehema kwa Mungu.
Upumbafu ni furaha kwa mutu asiyekuwa na akili, lakini mwenye akili anachagua njia inayokuwa sawa.
Usishuhudie bure juu ya jirani yako, wala usiseme uongo juu yake.
Vilevile kusisikilike maneno ya matusi ya ovyo ovyo wala machafu, kwa maana hayana mafaa. Kinachofaa ni kumushukuru Mungu.
Watalipwa mateso kwa sababu ya mateso waliyoleta. Wanafurahia kutimiza waziwazi tamaa zao mbaya za kimwili muchana kati. Kufika kwao katika karamu zenu kunaleta haya na chukizo kubwa wanapofurahia mambo yao ya udanganyifu.