Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.
Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.
Halafu akamugeukia yule mwanamuke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamuke huyu? Niliingia ndani ya nyumba yako, nawe haukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini mwanamuke huyu amenawa miguu yangu na machozi yake na kuipanguza na nywele zake.
Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.