Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 24:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa mupumbafu hekima ni ngumu kuielewa; penye mukutano wa mashauri hafungui mudomo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 24:7
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama nimekunjia yatima ngumi katika tribinali nikijua nitapendelewa na waamuzi,


Watoto wake hawana usalama. Wanaonelewa katika tribinali, na hakuna mutu wa kuwatetea.


Njia za mwovu zinafanikiwa siku zote; hukumu zako ziko mbali na mawazo yake, na anazarau waadui zake wote.


Heri mutu anayekuwa na mishale hiyo kwa wingi. Hatashindwa atakaposamba na waadui zake kwenye tribinali.


Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.


Njia ya mwenye hekima inaelekea juu kwenye uzima, kusudi aepuke kuingia chini katika kuzimu.


Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?


Hekima ni mbele ya uso wa mwenye akili, lakini macho ya mupumbafu yanaangalia kwa miisho ya dunia.


Maneno mazuri hayastahili katika kinywa cha mupumbafu, zaidi sana maneno ya uongo katika kinywa cha kiongozi!


Usinyanganye masikini mali yake kwa sababu ni masikini, wala usimunyime mukosefu haki yake katika tribinali.


Waovu hawaelewi haki ya sheria, lakini wanaomwogopa Yawe wanaielewa kabisa.


Mume wake ni mutu mwenye kuheshimiwa katika baraza, anapoikaa katikati ya wazee wa inchi.


Watatoweka wale wanaopotosha maneno ya mutu katika tribinali, watu wanaowatega waamuzi na wanaosema uongo kwa kuwanyima haki yao wasiokuwa na kosa.


Wapumbafu wanasema maneno ya upumbafu, na mafikiri yao ni kutenda maovu, kutenda mambo ya watu wasiomujua Mungu, kusema maneno ya kumutukana Yawe. Wanawaacha wenye njaa bila chakula, na wenye kiu wanawanyima kinywaji.


Ninyi munawachukia wanaotetea haki na wenye kusema ukweli katika tribinali.


Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ