Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 24:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 maana mutu wa haki anaanguka mara nyingi naye anainuka tena, lakini mutu mwovu anaangamizwa na hasara.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 24:16
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, usiku ule vilevile wakamulewesha baba yao kwa divai, kisha yule binti mudogo akakwenda akalala naye. Lakini baba yake hakujua wakati binti yake alipolala naye, wala wakati alipoondoka.


Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.


Atakuokoa mara sita toka katika magumu; hata mara saba hasara haitakugusa.


Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo; anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa.


Analinda viungo vya mwili wake wote, hakuna hata mufupa wake mumoja utakaovunjwa.


Hata akianguka, hatabaki chini, kwa sababu Yawe anamuimarisha.


Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri, unapenda uongo kuliko ukweli.


Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


Mujumbe mubaya anawatumbukiza watu katika taabu, lakini mujumbe mwaminifu analeta amani.


Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


maana maangamizi yatawatokea kwa rafla. Hakuna anayejua magumu watakayoleta.


Kutokana na hayo hasara itamupata kwa rafla; kwa rafla atapondekana vibaya wala hatapata kupona.


Nitawasambaza mbele ya waadui zao, kama upepo mukali toka mashariki. Nitawageuzia mugongo pahali pa kuwaelekezea uso siku hiyo watakapopatwa na hasara yao.


Wewe Yeremia utawaambia kwamba: Yawe anasema hivi: Mutu akianguka, hasimami tena? Mutu akipotea, harudii tena katika njia yake?


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mutapatwa na hasara! Hasara isiyoonekana bado!


Umeanguka na hautainuka tena ewe binti Israeli! Umeachwa ukiwa katika inchi yako, hakuna hata mutu wa kukuinua.


Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.


Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Kama vile Yawe anavyoishi, Yawe mwenyewe atamwua, au siku yake ya kufa itamufikia au atakuja kwenda katika vita na kuangamizwa kule.


Halafu Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wapagani wasikuje kunichoma upanga na kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakusubutu kwa sababu aliogopa sana. Kwa hiyo, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe, na kuuangukia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ