1 Usiwaonee wivu watu waovu, wala usitamani kuwa pamoja nao,
Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;
Usiniangamize pamoja na wenye zambi, wala usinitupe pamoja na wauaji,
Zaburi ya Daudi. Usihangaike kwa sababu ya waovu; usiwaonee wivu wanaotenda mabaya.
Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.
maana niliwaonea wivu wenye kiburi, nilipoona wakosaji wakifanikiwa.
Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.
Moyo wako usiwaonee wivu wenye zambi, lakini endelea kumwogopa Yawe siku zote.
Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya, wala usiwaonee wivu watu waovu,
Usimwonee wivu mutesaji, wala usiige mwenendo wake.
Usijiingize katika njia ya waovu, wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.
Epuka njia hiyo wala usiikaribie; ujiepushe nayo, uende zako.