Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 23:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 23:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anakwenda kulala akiwa tajiri, lakini ni mara ya mwisho; atafungua macho yake, na utajiri wake umetoweka!


Anayetamani faida ya unyanganyi anataabisha jamaa yake, lakini anayechukia kituliro ataishi.


Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.


Maana utajiri haudumu milele, wala taji haidumu kwa vizazi vyote.


Mutu mwaminifu atapata baraka tele, lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepuka azabu.


Umutumainie Yawe kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili zako mwenyewe.


Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima; umwogope Yawe na kujiepusha na uovu.


Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.


Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.


Yawe anasema hivi: Mwenye hekima asijivunie hekima yake, mwenye nguvu asijivunie nguvu yake; wala tajiri asijivunie utajiri wake.


“Musijiwekee akiba katika dunia hii, pahali nondo na kutu vinapoharibu, nao wizi wanapotoboa nyumba na kuiba.


lakini masumbuko ya dunia hii, udanganyifu wa mali, na tamaa za namna nyingine vikiwaingia, vinasonga lile Neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.


Mukuwe na masikilizano kati yenu. Musikuwe na nia ya kujitukuza, lakini mukubali kuishi katika unyenyekevu. Musijiwazie kuwa wenye akili sana.


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ