16 Moyo wangu utashangilia, midomo yako itakaposema maneno ya usawa.
Moyo wako usiwaonee wivu wenye zambi, lakini endelea kumwogopa Yawe siku zote.
Musikilize maana nitakachosema ni jambo la lazima; katika midomo yangu mutatoka mambo ya haki.
Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.
Vilevile kusisikilike maneno ya matusi ya ovyo ovyo wala machafu, kwa maana hayana mafaa. Kinachofaa ni kumushukuru Mungu.
Basi muniombee kusudi nipate kuupasha waziwazi sawa ninavyopaswa kufanya.
Sisi wote tunakosa kwa njia mbalimbali. Mutu asiyekosa katika masemi yake, huyo ni mutu mukamilifu, naye yuko na uwezo wa kutawala mwili wake wote.