13 Usiache kufundisha mutoto; ukimupiga fimbo hatakufa.
Asiyemwazibu mutoto wake hamupendi; lakini anayemupenda mwana wake atamwazibu kwa wakati.
Azibu mwana wako wakati kungali bado tumaini lakini usitafute kumwangamiza.
Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mutoto, lakini fimbo ya kufundisha itaufukuza mbali.
Tumia akili yako kwa kufuata mafundisho; tumia masikio yako kwa kusikiliza maarifa.
Azabu na maonyo vinaleta hekima, lakini mutoto aliyeachiliwa anapatisha mama yake haya.
Umwazibu mwana wako naye hatakupa wasiwasi; yeye atafurahisha moyo wako.
Muvumilie maadibisho; kwa maana Mungu anawatendea ninyi kama wana wake. Tena, ni mwana gani asiyeazibiwa na baba yake?