11 maana Mungu, Mukombozi wao, ni mwenye nguvu, naye atatetea haki yao nawe utaonekana kuwa na kosa.
Ninajua wazi Mukombozi wangu anaishi. Kwa mwisho yeye atasimama hapahapa katika dunia.
Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”
Mungu anayekaa pahali pake patakatifu, ni Baba ya wayatima na mulinzi wa wajane.
Maana Yawe atawatetea; atagandamiza maisha ya wale wanaowagandamiza.
Tumia akili yako kwa kufuata mafundisho; tumia masikio yako kwa kusikiliza maarifa.
Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawatetea juu ya maneno yenu, na kulipiza kisasi kwa ajili yenu. Nitaikausha bahari ya Babeli na kuvifanya visima vyake vikauke.
“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’