Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 22:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ukinyenyekea na kumwogopa Yawe, utapata zawadi ya fanaka, heshima, na uzima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 22:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kumwogopa Yawe kunaongoza kwenye uzima; anayemwogopa anajaliwa pumziko la kutoshelea, wala hatapatwa na ubaya wowote.


Katika nyumba ya mwenye hekima kuna hazina za bei kali, lakini mupumbafu anaponda mali yake yote.


Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.


Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.


Njia ya waovu imejaa miiba na mitego; anayetaka kulinda maisha yake ataiepuka.


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Mapendezi ni udanganyifu na uzuri wa uso haukawii, lakini mwanamuke anayemwogopa Yawe atasifiwa.


Enyi watu wa Yerusalema, Yawe atawajalia usalama, atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa. Akiba yenu kubwa ni kumwogopa Yawe.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


Mujinyenyekeze mbele ya Bwana, naye atawainua.


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ