Nitamwambia Yawe kwa moyo wangu wote: “Wewe, ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe! Wewe unawaokoa wamasikini kutoka makucha ya wenye nguvu, wamasikini na wakosefu kutoka mikono ya wanyanganyi.”
Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa vilevile, na waadui zako wote watapelekwa katika uhamisho; nao wanaokukamata mateka watakamatwa mateka, nao wanaokuwinda, nitawawinda.
Lakini mimi, Mukombozi wao ni mwenye nguvu. Yawe wa majeshi ndilo jina langu. Hakika nitatetea maneno yao kusudi nilete amani katika inchi yao, lakini taabu kwa wakaaji wa Babeli.
Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawatetea juu ya maneno yenu, na kulipiza kisasi kwa ajili yenu. Nitaikausha bahari ya Babeli na kuvifanya visima vyake vikauke.
Kwa vile nimemukosea Yawe, nitavumilia kasirani yake, mpaka atakapotetea maneno yangu na kunijalia haki yangu. Atanileta inje kwenye mwangaza, nami nitaona akisimamisha haki.
Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.
Angalia, baba yangu, angalia pindo hili la nguo yako katika mikono yangu. Kwa kulikata pindo la nguo yako bila kukuua, unaweza sasa kujua kwa hakika kwamba mimi si mwovu wala mwasi. Mimi sijatenda zambi juu yako ingawa wewe unaniwinda uniue.
Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.