Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 22:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Wewe utafurahi kama utayaweka ndani ya moyo, na kuyarudiliarudilia kila wakati.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 22:18
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maagizo yako ni matamu sana kwangu; ni matamu kuliko asali!


Maagizo yako ni urizi mukubwa kwangu milele; hayo ni furaha ya moyo wangu.


Nitarudiliarudilia kwa sauti maamuzi yako yote uliyotoa.


Ninafurahi kwa sababu ya neno lako, kama mutu aliyekuta kitu cha bei kali.


Midomo yangu itatangaza sifa zako, maana unanifundisha masharti yako.


Kumutii Yawe ni jambo jema; kunadumu milele. Maagizo ya Yawe ni sawa, yote ni ya haki kabisa.


Katika kinywa cha mwenye ufahamu kuna hekima, lakini wasiokuwa na akili watapigwa fimbo katika mugongo.


Maneno ya mwenye haki yanawafalia watu wengi, lakini wapumbafu wanakufa kwa kukosa akili.


Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.


Mwenye hekima ndani ya moyo anaitwa mwenye akili; neno la kupendeza linawavuta watu.


Maana hekima itaingia ndani ya moyo wako, na maarifa yatapendeza nafsi yako.


Ninayependa kumufundisha leo ni wewe, kusudi tumaini lako likuwe kwa Yawe.


Neno linalosemwa kwa wakati unaofaa, ni kama michoro ya zahabu juu ya feza.


Njia zake ni za kupendeza, zote zinaelekea kwenye amani.


Mwana wangu, sikia kwa uangalifu maneno yangu, utegee sikio masemi yangu.


Usiyaache yatoweke mbele ya macho, uyafunge ndani ya moyo wako.


Musikilize maana nitakachosema ni jambo la lazima; katika midomo yangu mutatoka mambo ya haki.


Palepale maneno yako yaliponifikia, niliyameza; nayo yakanifurahisha, yakakuwa matamu katika moyo wangu, maana mimi ninajulikana kwa jina lako, ee Yawe wa majeshi.


Ni kazi ya makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu kusudi watu wawaendee kwa kujifunza mapenzi yangu kwao, maana makuhani ni wajumbe wa Yawe wa majeshi.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: ‘Mito ya maji ya uzima yatatiririka toka ndani ya yule anayeniamini.’ ”


Basi kwa njia ya Yesu, tumutolee Mungu sadaka za kumusifu siku zote, maana yake kutangaza kwamba tunaaminia jina lake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ