Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 21:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 21:4
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kweli, mwangaza wa mutu mwovu utazimishwa; ulimi wa moto wake hautaangaa.


Katika nyumba yake mwangaza ni giza, taa inayomwangazia itazimishwa.


Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.


Nitateketeza yule anayemuteta mwenzake, sitamuvumilia mwenye majivuno na kiburi.


Wimbo wa safari za kidini: wa Daudi. Ee Yawe, sina moyo wa majivuno; wala macho yangu si ya kiburi. Sijishugulishi na mambo makubwa, yale yanayokuwa ya ajabu sana kwangu.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


maana siku mbaya zitamufikia mwovu; taa ya uzima wake itazimika.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Kuna vitu sita Yawe anavyochukia, hata saba ambavyo ni chukizo kwake:


Macho ya kiburi, ulimi mudanganyifu, mikono inayoua wasiokuwa na kosa,


Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Yawe anasema: Wanawake wa Sayuni wako na kiburi; wanatembea wakiinua kichwa juu, wakirembua macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, nao wanalilisha mikufu kwenye miguu yao.


Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako likiwa zima, mwili wako wote utabaki katika mwangaza. Lakini kama jicho lako linaharibika, mwili wako vilevile utabaki katika giza.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Lakini mutu anayekuwa na mashaka juu ya chakula anachokula, Mungu anamuhukumu, kwa sababu hatendi kufuatana na imani. Na kitendo chochote kisichotokana na imani ni zambi.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ