Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 21:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Moyo wa mufalme ni kama maji yanayotiririka; Yawe anauongoza popote anapopenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 21:1
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atarudi kwa njia ileile aliyokuja nayo wala hataingia katika muji huu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, Yawe akatimiza neno alilosema kwa njia ya nabii Yeremia. Yawe akaamusha nia ya Kiro mufalme wa Persia, naye akatoa amri hii katika ufalme wake, vilevile amri hiyo ikatolewa kwa maandiko:


Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.


Kwa muda wa siku saba watu walisherehekea kwa furaha sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa sababu Yawe aliwajalia furaha na kumupa mufalme wa Asuria moyo wa upendo kwao, akawasaidia katika kazi za ujenzi wa nyumba ya Mungu, wa Israeli.


Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.


Halafu mufalme Artasasta akanijibu: “Sasa unaomba nini?” Nikamwomba Mungu wa mbinguni.


Vilevile ninakuomba kwamba barua ingine iandikwe kwa Asafu mulinzi wa pori la kifalme kusudi anipatie mbao za kutengeneza miimo ya milango ya munara wa hekalu, ukuta wa muji na nyumba yangu nitakamokaa.” Mufalme akakubali ombi langu kwa kuwa Mungu, kwa wema wake, alikuwa pamoja nami.


Mufalme akamupenda zaidi Esteri kuliko wanawake wote. Naye Esteri akapata kukubaliwa na kutendewa mema mbele yake zaidi kuliko wabinti wengine wote. Basi, mufalme akamuvalisha taji ya kimalkia kwenye kichwa, akamufanya malkia pahali pa Vashiti.


Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake, wakawatendea watumishi wake vibaya.


Aliwafanya wale waliowaangamiza wawaonee huruma.


Bahari iliona hayo ikakimbia; muto Yordani ukaacha kutiririka!


Ee bahari, nini iliyokufikia hata ukakimbia? Nawe Yordani, kwa nini uliacha kutiririka?


Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa.


Yawe ana mamlaka juu mbinguni, ana nguvu kuliko mulio wa bahari, ana nguvu kuliko mawimbi ya maji.


Lakini nitafanya moyo wa mufalme kuwa mugumu. Na hata kama nitazidisha vitambulisho na maajabu yangu katika inchi ya Misri,


Mwanadamu anapanga mipango yake, lakini neno la mwisho ni la Yawe.


Mutu anaweza kufanya mipango yake, lakini Yawe anaongoza hatua zake.


Hatua za mutu zinaongozwa na Yawe; mwanadamu anaweza namna gani kuelewa njia yake?


Muangalie, mimi ninafanya kitu kipya. Kinafanyika sasa hivi, nanyi mutaweza kukiona. Nitafanya njia katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa.


Mimi ndiye ninayeviamuru vilindi: Mukauke, nitakausha mito yenu.


Umutwae Yeremia, umutunze vema wala usimuzuru; umutendee kama anavyokuambia.


akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.


Malaika wa sita akamwanga kikombe chake katika muto mukubwa Furati. Maji yake yakakauka kusudi njia itengenezwe kwa ajili ya wafalme wanaotoka mashariki.


Malaika wa tatu akamwanga kikombe chake katika mito na chemichemi za maji, na maji yao yakageuka damu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ