Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 20:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Heri watoto wa mutu wa haki mwenye mwenendo mukamilifu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 20:7
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.


Kulikuwa mutu mumoja katika inchi ya Usi, aliyeitwa Yobu. Mutu yule alikuwa mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.


Wazao wake watakuwa wenye nguvu katika inchi; watoto wa watu wa usawa watapata baraka.


Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.


Zaburi ya Daudi. Ee Yawe, unitetee, maana nimeishi katika ukamilifu, nimekutumainia wewe bila kusita.


Lakini mimi ninaishi katika ukamilifu; unihurumie na kunikomboa.


Siku zote yeye anakopesha kwa moyo safi, na watoto wake ni wenye baraka.


Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.


Mwenye mwenendo sawa anamwogopa Yawe, lakini mupotovu anamuzarau Mungu.


Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.


Afazali masikini mwenye mwenendo mukamilifu kuliko mutu mupotovu wa maneno na mupumbafu.


Ni mutu anayekuwa hivi: anaishi kwa haki na kusema kwa usawa, anazarau kabisa utajiri wa unyanganyi, anakataa kupokea kituliro, hakubali hata kidogo kusikia mipango ya mauaji, wala hakubali macho yake yaone maovu.


Nitawapa moyo mumoja na nia moja, wapate kuniheshimu mimi siku zote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao watakaofuata.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ