Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 20:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Watu wengi wanajivunia kuwa wema, lakini mwaminifu wa kweli anapatikana wapi?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 20:6
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.


Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu.


Mafikiri ya mutu ndani ya moyo wake ni kama kilindi cha maji; lakini mutu mwenye akili anajua kuyachota mule.


Kama vile mawingu na upepo bila mvua, ndivyo anavyokuwa mutu anayeahidi zawadi na haitoi.


Acha watu wengine wakusifu, kuliko kujisifu kwa mudomo wako wewe mwenyewe.


Niliendelea kutafuta mambo hayo, lakini sikupata. Kati ya wanaume elfu moja, nilipata kuona mwanaume mumoja anayestahili heshima, lakini kati ya wanawake wote, sikuona hata mumoja anayestahili heshima.


Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.


Ole wangu! Mimi ninakuwa kama muvunaji kisha wakati wa mavuno; hakuna tini za kwanzakwanza ninazotamani. Ni kama wakati wa kuchuma zabibu: hakuna hata fungu moja la zabibu la kula!


Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.


“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.


Basi Petro akamwambia: “Sisi tumeacha vyote tulivyokuwa navyo na kukufuata wewe!”


Ninawaambia ninyi: hatakawia kuwapatia haki. Lakini Mwana wa Mutu atakaporudia, atakuta watu wenye kumwamini katika dunia?”


Petro akamwambia: “Bwana, mimi niko tayari kufungwa pamoja nawe na hata kufa pamoja nawe.”


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


Ninasema kama mupumbafu, lakini ni ninyi ndio mumenilazimisha kufanya vile. Kufuatana na ile, ningepaswa kusifiwa nanyi. Kwa maana hata kama mimi si kitu, wale mitume wenu wanaohesabiwa kuwa wakubwa hawanipiti kitu kabisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ