4 Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.
Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.
Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.
Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.
Muvivu anatia mukono wake katika sahani lakini hauinui mpaka kwenye midomo.
Mafikiri ya mutu ndani ya moyo wake ni kama kilindi cha maji; lakini mutu mwenye akili anajua kuyachota mule.
Muvivu anakufa kwa kutokutimizwa kwa tamaa zake, maana mikono yake haitaki kufanya kazi.
lakini kumbuka kwamba unapokuwa katika usingizi, umasikini utakufikia kama munyanganyi, ukosefu kama mutu mwenye silaha.
Ewe muvivu! Kwenda kuchunguza siafu, fikiri juu ya namna yake ya kuishi upate hekima.
Anayechunguza upepo hatapanda mbegu, anayeangalia mawingu yatoweke, hatavuna kitu.