2 Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.
Hapo mufalme Solomono akaapa kwa jina la Yawe, akisema: “Mungu aniue ikiwa Adonia hatakufa kwa sababu ya kutoa ombi hili!
Sasa basi, kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyeniweka na kuniimarisha katika ufalme wa baba yangu Daudi na kutimiza ahadi yake ya kunipa kiti cha kifalme mimi na wazao wangu, Adonia atakufa leo!”
Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.
Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”
Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.
Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.
Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?
Lakini kwa mipango yako umefezehesha jamaa lako. Kwa kuyaangamiza mataifa mengi, umeyaangamiza maisha yako mwenyewe.